Wapenzi wa soka hapo jana nchini Brazili walishuhudia tukio lisilo la kawaida katika mchezo wa soka baada ya derby timu za Vitoria na Ba...
Wapenzi wa soka hapo jana nchini Brazili walishuhudia tukio lisilo la kawaida katika mchezo wa soka baada ya derby timu za Vitoria na Bahia kumalizika kwa vurugu dakika za lala salama.
Vurugu hizo ziliibuka zikiwa zimesalia dakika 13 kabla ya mchezo huo kumalizika baada ya mchezaji wa Bahia kusheherekea goli akiwa ameisawazishia bao timu hiyo na kuwa sawa kwa mabao 1 – 1.
Kufuatia bao hilo la penati ndipo wachezaji wa timu mwenyeji ambayo ni Vitoria waaanza kumshambulia mchezaji huyo hadi kupelekea mwamuzi wa mchezo huo kutoa kadi hizo 10 nyekundu dakika ya 77 namchezo huo kumalizikia hapo.
Katika kadi hizo jumla ya wachezaji nane walipata kadi nyekundu za moja kwa moja ambapo kwa upande wa timu ya Victoria waliyolimwa kadi hizo wakiwa watatu na
Katika mchezo huo jumla ya wachezaji nane walipata kadi nyekundu za moja kwa moja ambapo kwa wa timu ya Victoria waliyolimwa walikuwa watatu huku kwa upande wa Bahia wakiwa watano.
Na wachezaji wengine nane kwa kila upande walijikuta wakipata kadi za njano kwa kushiriki vurugu hizo.
Mwenyeji wa mchezo huo ambao ni timu ya Vitoria inashika nafasi ya pili katika msimo wa ligi ya Brazili kwa kuwa na jumla ya pointi 10 wakati hasimu wake Bahia ikiwa nafasi ya tano kwakuwa na alama nane wakati nafasi ya kwanza ikishikiliwa na Juazeirense.
COMMENTS