Kesi za uchochezi na vitendo vya utekaji kwa Waandishi wa Habari vyaongezeka Uganda

Chama cha waandishi wa habari nchini Uganda kinalaani ongezeko la ukamatwaji kiholela wa Waandishi nchini humo na Jeshi la Polisi kisha ...


Chama cha waandishi wa habari nchini Uganda kinalaani ongezeko la ukamatwaji kiholela wa Waandishi nchini humo na Jeshi la Polisi kisha kufunguliwa kesi za uhaini na wengine kutekwa na watu wasiojulikana kisha kupelekwa magerezani bila kufikishwa mahakamani.

Taarifa hiyo iliyotolewa jana na chama hicho imejiri baada ya waandishi wa habari watatu wa gazeti wa Daily Monitor kukamatwa katika mazingira ya utatanishi na kushtakiwa kwa njama ya kujaribu kuipindua serikali, mashtaka ambayo adhabu yake ni kifo endapo watakutwa na hatia.

Nchini Uganda kumekuwa na ripoti za waandishi wa habari kutekwa na watu wasiojulikana na kisha baadaye kupatikana gerezani wakiwa wamefungwa bila hatia kumezua hofu kubwa kwa waandishi wa habari.

Jana Jumatatu Februari 19, 2018 mwandishi wa habari wa kituo cha habari cha kibinafsi cha Top Radio, Richard Kasule alikamatwa nje ya ofisi za kituo hicho muda mfupi baada ya kuandaa matangazo ya asubuhi.

Wafanayakazi wenzake katika kituo hicho cha habari walidai kwamba Kasule alikamatwa na polisi baada ya kufichua ushirikiano kati ya walinda usalama na makundi ya uhalifu jijini Kampala.
Mtangazaji huyo aliandaa kipindi cha saa nzima akiwahoji viongozi wa makundi hayo ya uhalifu waliodai kushirikiana na polisi katika uhalifu.

Hatua ya kukamatwa kwa kasule inajiri siku mbili baada ya mwandishi wa gazeti la serikali la the New Vision, Charles Etukuri, kukamatwa nje ya ofisi za gazeti hilo la serikali.
Etukuri alichapisha taarifa ya upekuzi kuhusiana kifo cha mwekezaji kutoka bara la Ulaya katika hoteli moja maarufu jijini Kampala, na kukamatwa kwa viongozi wakuu 6 wa polisi kisiri.
Mwandishi mwingine wa habari, Isaac Bakka, alipatikana gerezani baada ya kutoweka katika mazingira ya kutatanisha wiki mbili zilizopita.

Hata hivyo, Mahakama jijini Kampala kupitia Mkurugenzi wa Habari, Solomon Muyita, amesema mwandishi huyo alikuwa ameshafunguliwa mashtaka ya uagizaji wa silaha hatari kwa nia ya kuipindua serikali ya Yoweri Museveni.

Wahariri wa gazeti la upekuzi la Red Pepper, Juice FM na gazeti linalochapishwa kwa lugha ya kiganda la ‘Kamunye,’ nao wanakabiliwa na mashtaka ya kujaribu kuipindua serikali ya rais Yoweri Museveni.

Vituo hivyo vimefunguliwa hivi majuzi baada ya kufungiwa kwa mda wa mwezi mmoja kwa makosa ya kuandika habari za kichochezi na zenye lengo la kuvuruga amani nchini humo.

Chanzo:VOA

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: Kesi za uchochezi na vitendo vya utekaji kwa Waandishi wa Habari vyaongezeka Uganda
Kesi za uchochezi na vitendo vya utekaji kwa Waandishi wa Habari vyaongezeka Uganda
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhGQP58jIuL1qnVU-E57xwnFog5ZqkbTNEyhb_rLNEtK0IZvbQN-Np_Ep24DoNRzcmnLOFfU9-fwjPuqDbiCaaW1TRLigsAiAYwEqMHopfFXEZDIdGcrVQ35UWUgUuojtrPHPCdB-f34G1P/s640/bariiiiiii.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhGQP58jIuL1qnVU-E57xwnFog5ZqkbTNEyhb_rLNEtK0IZvbQN-Np_Ep24DoNRzcmnLOFfU9-fwjPuqDbiCaaW1TRLigsAiAYwEqMHopfFXEZDIdGcrVQ35UWUgUuojtrPHPCdB-f34G1P/s72-c/bariiiiiii.jpg
Habari Today
https://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/kesi-za-uchochezi-na-vitendo-vya.html
https://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/kesi-za-uchochezi-na-vitendo-vya.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy