Jinsi Ya Kukubaliana Na Ukosefu Wa Hamu Ya Tendo La Ndoa Kwa Wanawake

KUKOSA hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke kunaweza kutafsiriwa kwa aina tatu, ambazo ni kutopata hamasa ya kufanya tendo la ndoa hata b...


KUKOSA hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke kunaweza kutafsiriwa kwa aina tatu, ambazo ni kutopata hamasa ya kufanya tendo la ndoa hata baada ya kuchochewa; kuepuka kufanya tendo la ndoa ukiwa kwenye mahusiano bila sababu ya msingi; kushiriki tendo la ndoa bila kufurahia na bila kufi kia kilele.
Tatizo hili linaweza kuleta kutokuelewana baina ya wenza na ni chanzo kimojawapo cha mafarakano kwenye mahusiano. Kama ilivyo kwenye ukosefu wa nguvu za kiume, kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa wanawake kunasababishwa na matatizo ya kiafya au ya kisaikolojia.

Kunaweza kutokea baadhi ya nyakati kwa muda mfupi; lakini endapo tatizo hilo linakuwa endelevu kiasi cha kusababisha matatizo kwenye uhusiano ni vizuri kutafuta ushauri wa kitaalamu.
Mara nyingi kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake kunaletwa na adha au maudhi fulani ambayo yametokea na hayajazungumziwa baina ya wenza au kutafutiwa ufumbuzi.

 Hivyo, ushauri wa kwanza ni kuwa na mawasiliano ya wazi ili kurekebisha yale yanayowezekana.

 Tendo la ndoa kwa mwanamke linahusisha vitu vingi lakini hasa ni matayarisho ya kutosha yanayoleta hisia na vitendo vinavyoonesha kupendwa, kuthaminiwa na hali ya kuwa salama.
Hamu ya tendo la ndoa haiji tu mara moja pale ambapo mwenza mmoja amejisikia, bali mazingira lazima yawe sahihi na mazuri ili wote kufurahia.

 Sababu za kisaikolojia zinazoleta kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa mwanamke ni kama vile historia ya kufanyiwa vitendo viovu kama kubakwa, kutokuwa karibu na mwenza kifikra, mawasiliano hafifu na migogoro ya mara kwa mara kwenye uhusiano.
Sambamba na sababu hizo ni mazingira yasiyo rafiki kwa mfano uwepo wa watoto au mkwe chumba cha karibu, pamoja na mwenza aliyelewa.

Zipo pia sababu za kiafya ambazo ni pamoja na maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa, upungufu wa nguvu za kiume kwa mwenza, baadhi ya dawa, pombe na mabadiliko ya homoni hasa pale mtu anapokaribia kukoma hedhi.
Hatua ya kwanza ya kuchukua endapo una tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa ni kutafuta ushauri wa kitaalamu ili kubaini endapo tatizo lako ni la kiafya au la kisaikolojia. Mtaalamu wa afya atatoa ushauri kulingana na tatizo atalogundua.
Asilimia kubwa ya matatizo ya kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa mwanamke yanaletwa na sababu za mahusiano, hivyo basi hatua ya muhimu katika kukabiliana na tatizo hili ni kujadiliana na kufikia muafaka wa mambo yanayowatatiza kama vile kukosa muda wa kukaa pamoja, mahusiano ya kimapenzi na mtu mwingine ambayo yanaweza kuwa mapya au ya zamani na malumbano ya mara kwa mara.

 Ni muhimu kufahamu pia kuwa baadhi ya mambo nje ya mahusiano yanaweza kuleta madhara kama vile matatizo ya kifedha au matatizo kazini.

Yote haya yanasababisha kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa na hivyo ni muhimu sana kutafuta wataalamu wa ushauri ili kuweza kuzungumzia mambo haya na kupata mbinu za jinsi ya kukabiliana nayo.

Kwa wale wenye shida za homoni zinazosababisha kukosa hamu ya tendo la ndoa, mtaalamu wa afya atashauri njia bora ya tiba ikiwa ni pamoja na kukupatia dawa za kurekebisha hali hiyo.

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: Jinsi Ya Kukubaliana Na Ukosefu Wa Hamu Ya Tendo La Ndoa Kwa Wanawake
Jinsi Ya Kukubaliana Na Ukosefu Wa Hamu Ya Tendo La Ndoa Kwa Wanawake
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhs5s5Pu_GANrWudD_IHalFq8alxPf7N9JL0FRkVcgRTp6LUyubJUSYo1zIdV-ECLoY8UHTeJWrrF38Yjg1VOm4bEvQsQVnJymz1_d2yAINWnpLss20w-DNix2l-44gdek-rtkUuBxqHpnE/s640/ndoa.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhs5s5Pu_GANrWudD_IHalFq8alxPf7N9JL0FRkVcgRTp6LUyubJUSYo1zIdV-ECLoY8UHTeJWrrF38Yjg1VOm4bEvQsQVnJymz1_d2yAINWnpLss20w-DNix2l-44gdek-rtkUuBxqHpnE/s72-c/ndoa.jpg
Habari Today
https://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/blog-post.html
https://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/blog-post.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy