Aliyekuwa Kamishna Wa Madini Afikishwa Mahakamani Kwa Matumizi Mabaya Ya Madaraka

Aliyekuwa Kaimu Kamishna wa Madini, Ally Bondo Samaje amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka mawili ya mat...


Aliyekuwa Kaimu Kamishna wa Madini, Ally Bondo Samaje amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka mawili ya matumizi mabaya ya madaraka.

Samaje amefikishwa katika mahakamani hiyo jijini Dar es Salaam leo Februari 9, 2018.

Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambna na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo, April 9, 2013 na Juni 21, 2013 Makao makuu ya Wizara ya Nishati na Madini.

Amesema akiwa Kaimu Kamishna wa Madini, alitumia madaraka yake vibaya kwa kushindwa kuishauri Bodi ya Madini katika utoaji wa leseni ya madini ya Graphite na Marble kwa Kampuni ya Tanzaniteone Mining Limited na State Mining Corporation.

Katika shtaka la pili, April 16, 2013 makao Makuu ya Wizara ya Nishati iliyopo wilaya ya Ilala, akiwa Kaimu Kamishna wa Madini na Katibu wa Bodi ya Ushauri wa Madini kutoka wizarani, alitumia vibaya madaraka yake kwa kutoa maelekezo kwa msaidizi wake John Nayopa kuandaa leseni za madini ya Graphite and Marble, bila kufuata sheria ya madini.

Mshtakiwa yupo nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili na mmojawapo kusaini bondi ya Sh 50milioni.
Pia mshtakiwa hatakiwi kusafiri nje ya nchi bila kibali cha Mahakama.


Na Hadija Jumanne, Mwananchi

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: Aliyekuwa Kamishna Wa Madini Afikishwa Mahakamani Kwa Matumizi Mabaya Ya Madaraka
Aliyekuwa Kamishna Wa Madini Afikishwa Mahakamani Kwa Matumizi Mabaya Ya Madaraka
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiDuiRFgGcP4AYhAeoPG2weiFW6OYRZ5JzCTzVg5T9ZWCmyQwDPcinwdokP5HTMsGCiQN9qsLXCYTIU_rW1luSFLvck0z0GzhM1UtjbMK9hytoSBHZNUqKy92xjhItR5vLk9Yzm7jFzVQ5o/s640/madini.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiDuiRFgGcP4AYhAeoPG2weiFW6OYRZ5JzCTzVg5T9ZWCmyQwDPcinwdokP5HTMsGCiQN9qsLXCYTIU_rW1luSFLvck0z0GzhM1UtjbMK9hytoSBHZNUqKy92xjhItR5vLk9Yzm7jFzVQ5o/s72-c/madini.jpg
Habari Today
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/aliyekuwa-kamishna-wa-madini-afikishwa.html
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/aliyekuwa-kamishna-wa-madini-afikishwa.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy