Baba mzazi wa ‘Akwilina’ amlilia polisi aliyemuua mwanaye ‘nitapambana naye hata kumuua kwa meno’

Mzee Akwilini Shirima (Picha na Mwananchi) Kwa mara ya kwanza Baba mzazi wa mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwi...


Mzee Akwilini Shirima (Picha na Mwananchi)

Kwa mara ya kwanza Baba mzazi wa mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini ambaye ameuawa na askari polisi kwa kupigwa risasi siku ya Ijumaa ya wiki iliyopita, Mzee Akwilini Shirima ameongea na kueleza hisia zake kwa askari aliyetekeleza mauaji ya mwanaye akidai kuwa endapo akikutana naye atapambana naye hadi kifo.

Mzee Shirima amesema endapo muuaji atakuwa ni kijana mwenye nguvu kumzidi yeye, atapambana naye hata kwa kumuuma kwa meno ili mradi tu afanikiwe kumtoa uhai.

Najua ni ngumu kukutana na aliyempiga mwanangu risasi, lakini laiti ningekutana naye kama ni kijana mwenye nguvu kunizidi nitapambana naye hata kumuuma kwa meno.. Kama ni mzee mwenzangu nitapambana naye hadi kifo ila kwa bahati mbaya siwezi kumpata, hivyo sina namna,“amesema Mzee Shirima kwenye mahojiano yake na Gazeti la Mwananchi.

Kwa upande mwingine Mzee Shirima amesema kuwa kifo cha mwanaye kimezima ndoto ya familia yake kuondokana na umasikini huku akiiomba serikali kuliangalia suala hilo kwa kina na kuona namna ya kumsaidia kwa kuwa tegemeo lake limeondoka .

Jamani hii ni taa yangu imezimika na kuniacha gizani kwani toka nimepata taarifa za kifo chake sijaweza kula chochote. Nimekuwa kama nguruwe aliyetelekezwa porini bila msaada,“ameliambia gazeti hilo huku qkieleza jinsi alivyopokea taarifa hizo mbaya zaidi kwenye familia yake.

Nilipopata taarifa za kifo cha mwanangu nilishtuka sana na kuhoji ni mwizi au nini kimetokea, lakini baadaye nikaambiwa ni Serikali imefanya mambo hayo. Imenitia uchungu sana na siwezi hata kula,“amesema Mzee Shirima.


Akwilina alifariki dunia Februari 16, 2018 baada ya kupigwa risasi kichwani akiwa kwenye daladala wakati polisi wakiwatawanya waandamanaji ambao ni wafuasi wa Chadema.

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: Baba mzazi wa ‘Akwilina’ amlilia polisi aliyemuua mwanaye ‘nitapambana naye hata kumuua kwa meno’
Baba mzazi wa ‘Akwilina’ amlilia polisi aliyemuua mwanaye ‘nitapambana naye hata kumuua kwa meno’
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg3Nj0Nw7L1uVmU42Y2Gg0Ozm0ytLYtGlZm2mzPEj5Dq0eIE0OexmFnfHM-TP6psbN7HmFnzG6jcFH2tpquXmA_z41wMG8YUw3R6zBZ5zon5b-_qb3FBMB7UK6VJFmWuTXo4LCipesStm4Y/s640/baba.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg3Nj0Nw7L1uVmU42Y2Gg0Ozm0ytLYtGlZm2mzPEj5Dq0eIE0OexmFnfHM-TP6psbN7HmFnzG6jcFH2tpquXmA_z41wMG8YUw3R6zBZ5zon5b-_qb3FBMB7UK6VJFmWuTXo4LCipesStm4Y/s72-c/baba.jpg
Habari Today
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/baba-mzazi-wa-akwilina-amlilia-polisi.html
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/baba-mzazi-wa-akwilina-amlilia-polisi.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy