Makamu Wa Rais Atoa Neno Kuhusu Ujenzi Wa Vituo Vya Afya

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema Serikali inajitahidi kujenga na kutanua vituo vya Afya i...


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema Serikali inajitahidi kujenga na kutanua vituo vya Afya ikiwa na lengo la kupunguza msongamano kwenye hospitali za Wilaya.

Makamu wa Rais ameyasema hayo jana wakati wa kuweka jiwe la msingi la upanuzi wa kituo cha Afya Ihongole kilichopo mjini Mafinga.

Makamu wa Rais ambaye yupo kwenye ziara ya kuhamasisha shughuli za kimaendeleo mkoani Iringa ambapo jana alitembele wilaya ya Mufindi na kuweka mawe ya msingi katika miradi miwili ikiwa mmoja ni wa kujenga maabara ya kisasa na madarasa na kidato cha tano na cha sita katika Sekondari ya Mgololo na upanuzi wa kituo cha Afya cha Ihongole kilichopo Mafinga.
Akiwahutubia wananchi waliojitokeza kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi la Upanuzi wa kituo cha Afya Ihongole , Makamu wa Rais alisema katika kila kituo cha afya kinachopanuliwa ama kujengwa Serikali imezingatia huduma za mama na mtoto ili kupunguza vifo vya akinamama na watoto, kuborsha huduma za upasuaji .

Serikali imetoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya upanuzi wa kituo hicho na kutumia mafundi wa kawaida kujenga ilikuweza kusaidia kutoa ajira kwa vijana zaidi wa eneo husika.
Makamu wa Rais amezitaka halmashauri zisimamie utoaji na matumizi ya fedha wanazotoa kwa Vijana asilimia 5 na Wanawake asilimia 5 ili kuleta tija kwenye shughuli za maendeleo.
Makamu wa Rais alisema “Tunapozungumzia uchumi wa viwanda lazima tuwaandae Vijana tangia wadogo, tuhakikishe wanafundishwa yale yanayohitajika”.
Makamu wa Rais aliwaambia wakazi wa Mafinga, watakapokuja tena kwenye kampeni watawataka wananchi waseme Serikali yao imewafanyia nini.


Mapema jana Makamu wa Rais aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa maabara na madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya sekondari Mgololo, ujenzi ambao utagharimu shilingi milioni 450 za kitanzania chini ya ufadhili wa kiwanda cha Mufindi Paper Mills.

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: Makamu Wa Rais Atoa Neno Kuhusu Ujenzi Wa Vituo Vya Afya
Makamu Wa Rais Atoa Neno Kuhusu Ujenzi Wa Vituo Vya Afya
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXhg_ZTUfLMGHTXAiC2UYPlfZnLMxW0t9g5e6GgDa0hBfJU12Pyb5PaybKsKH4aa4YPGcqXPqwbAf1TeWmsm0JCegUeFfKgWaQGkMIO7GhXIDUIQav1SN1qvZmmxaCsAJ0NuosgTPUr1p7/s640/SULUHU.png
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXhg_ZTUfLMGHTXAiC2UYPlfZnLMxW0t9g5e6GgDa0hBfJU12Pyb5PaybKsKH4aa4YPGcqXPqwbAf1TeWmsm0JCegUeFfKgWaQGkMIO7GhXIDUIQav1SN1qvZmmxaCsAJ0NuosgTPUr1p7/s72-c/SULUHU.png
Habari Today
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/makamu-wa-rais-atoa-neno-kuhusu-ujenzi.html
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/makamu-wa-rais-atoa-neno-kuhusu-ujenzi.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy