Leo Februari 9, 2018 kuna hii ya kuifahamu kuhusu Mwanamke mmoja baada ya kunywa pombe na kulewa huku wakifurahia wakati waliokuwa nao,...
Leo Februari 9, 2018 kuna hii ya kuifahamu kuhusu Mwanamke mmoja baada
ya kunywa pombe na kulewa huku wakifurahia wakati waliokuwa nao, kwenye
Mji wa Bangkon nchini Thailand akiwa na rafiki yake amegongwa na
kupoteza maisha huku mwenzie akijeruhiwa vibaya baada ya kugongwa na
treni walipokuwa wanapiga ‘selfie’.
Rafiki huyo ambaye amejeruhiwa ameelezea mkasa huo na kusema walikuwa
wamekunywa pombe na kulewa na ndiyo Marehemu akamwambia wakapige picha
kwenye reli lakini hawakuwa wameona treni inayokuja upande mwingine.
Tukio hilo lilitokea katika kituo cha treni cha Samsen February 8, 2018
na inaelezwa kuwa binti huyo aliyefariki alikuwa ana miaka 24 na aliumia
vibaya mguu na alipoteza maisha akiwa anapatiwa matibabu hospitali.
COMMENTS