SPICE HOTEL LIMITED Viongozi wa Mtandao wa Kijani kibichi Tanzania (Mkikita), wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Dk. Kissui Stev...
Viongozi wa Mtandao wa Kijani kibichi Tanzania (Mkikita), wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Dk. Kissui Steven Kissui (Kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa mtandao huo, Adam Ngamange (wa nne kushoto), wakiwa nje ya Spice Hotel Limited, baada ya kufanya mkutano na waandishi wa habari hoteni hapo, Dar es Salaam jana
Uongozi
wa Mkikita umefurahishwa na huduma za hoteli hiyo iliyopo makutano ya
mitaa ya Narung'ombe na Lumumba Karikaoo Dar es Salaam na kuahidi
mikutano mingine ijayo kuendelea kufanyia hapo.
Baada
ya kumaliza mkutano, uongozi wa Mtandao huo ulimtembelea Mmiliki wa
Hoteli Ofisi kwake, Bw. Mwangaba kwa lengo la kufahamiana pamoja na
kumpa pongezi kutokana na hoteli hiyo kuwapatia huduma nzuri.
Mwangaba
mwenye hoteli hiyo ya kisasa yenye vyumba 67 vyenye hadhi tofauti
alishukuru na kuwakaribisha tena kwenda hapo kwa shughuli mbalimbali.
Pia alikubali kujiunga na mtandao ili awe anashiriki kwenye shughuli
mbalimbali zinazofanywa na mtandao huo na kunufaika nazo pia. Kwa habari
zaidi kuhusu hoteli hiyo soma maelezo yaliyopo mwisho wa ukurasa huu.
Viongozi
wa Mkikita wakiwa katika picha ya pamoja na Mmiliki wa Hoteli ya Spice,
Mwangaba (wa pili kushoto). Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi, Dk.
Kissui S. Kissui, Meneja wa Mashamba, Catherina, Ofisa wa Logistic,
Morris Mwita, CEO Adam Ngamange, Ofisa Uhusiano, Neema Fredrick na
Meneja Masoko, Deo.
CEO
Adam Ngamange akizungumza katika mkutano na wanahabari, kuhusu
maandalizi ya mafunzo ya kilimo biashara cha Papai Salama kwenye ukumbi
wa mikutano wa hoteli hiyo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Hope For All, Askofu Edger Mwamfupe akizungumza
kuhusu makubaliano ya ushirikiano waliosaini na Mkikita kwa lengo la
kuwakomboa wananchi masikini Tanzania.
Mfanyabiashara Adamjee akielezea jinsi anavyokiendesha kwa faida kubwa kilimo cha pilipili kichaa
Mwenyekiti wa Bodi ya Mkikita, Dk. Kissui akizungumza katika mkutano huo, kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na mtandao huo.
Ofisa
Uhusiano wa Mkikita, Neema, akielezea utaratibu unaotumika kuwasajili
watu wanaotaka kuhudhuria mafunzo ya kilimo kibiashara cha Papai Salama
Mmiliki wa Spice Hotel, Mwangaba (kulia), akizungumza alipokutana na viongozi wa Mkikita kwa lengo la kufahamiana
COMMENTS