Baada ya kauli ya ‘Tanzania kichwa cha mwendawazimu kila mtu anaweza kujifunzia kunyoa’ kudumu kwa miaka 30, Hatimaye Rais Mstaafu wa aw...
Baada ya kauli ya ‘Tanzania kichwa cha mwendawazimu kila mtu anaweza kujifunzia kunyoa’ kudumu kwa miaka 30, Hatimaye Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi amekiri wazi kufuta kauli hiyo.
Mzee Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa kombe la
Shirikisho barani Afrika kati ya Simba SC dhidi ya Gendarmerie Tnale
kutoka Djibouti, alifuta kauli hiyo baada ya mchezo huo kumalizika.
”Nimeshuhudia mchezo mzuri na sasa nafuta lile neno kwamba Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu kila anaetaka kujifundisha kunyoa atunyoe sisi, sasa nyie ndio vinyozi.” alisema Mzee mwinyi kwenye mahojiano na vyombo vya Habari baada ya mchezo huo.
Klabu ya Simba jana ilifanikiwa kuwachabanga Gendarmerie Tnale goli 4-0 kwenye mchezo ambao ulikuwa wa kusisimua kwa mashabiki wa Msimbazi.
”Nimeshuhudia mchezo mzuri na sasa nafuta lile neno kwamba Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu kila anaetaka kujifundisha kunyoa atunyoe sisi, sasa nyie ndio vinyozi.” alisema Mzee mwinyi kwenye mahojiano na vyombo vya Habari baada ya mchezo huo.
Klabu ya Simba jana ilifanikiwa kuwachabanga Gendarmerie Tnale goli 4-0 kwenye mchezo ambao ulikuwa wa kusisimua kwa mashabiki wa Msimbazi.
COMMENTS