Nyota Hawa 20 Wa Yanga SC kuelekea Shelisheli Kesho Tayari Kuivaa St Louis, Chirwa ‘Out’

KIKOSI cha Yanga Sc kinatarajia kusafiri kesho asubuhi kueleka Shelisheli tayari kwa mchezo wa marejeano na wenyeji  St Louis Fc kwenye l...


KIKOSI cha Yanga Sc kinatarajia kusafiri kesho asubuhi kueleka Shelisheli tayari kwa mchezo wa marejeano na wenyeji  St Louis Fc kwenye ligi ya mabingwa afrika mchezo ulipangwa  kuchezwa Jumatano ijayo Stade Liete.

Muda mfupi  uliopita  Ofisa habari wa Yanga, Dismas Ten amesema kuwa jumla ya nyota 20 na viongozi 10 kati yao nane kutoka benchi la ufundi watasafiri asubuhi ya kesho  kupitia Nairobi tayari kwa mchezo huo muhimu  siku ya Jumatano.
Maandalizi yote muhimu yamekwisha fanyika, timu imefanya mazoezi ya mwisho leo tayari kwa safari hiyo. Kwenye kikosi nyota waliyokuwa na majeraha ya muda mrefu kama Amissi Tambwe, Donald Ngoma, Abdallah Shaibu na Yohana Mkomola wataendelea kukosekana hii ni kwa sababu bado wanauguza majeraha,kucheza ugenini  kunachangamoto zake lakini tumejiandaa vizuri kwa sababu tushacheza nje mara nyingi hivyo hakuna hofu kati yetu.
Akiendelea zaidi Ten amesema kuwa, mchezaji Thabani Kamusoko ambaye amepona majeraha yake hivi karibuni na kuanza mazoezi mepesi,ameondolewa kutoka orodha ya nyota ambao wangesafiri kueleka Shelisheli ili apate muda wa kujifua zaidi na kurejesha makali yake, mchezaji Obrey Chirwa  pia hayumo kwenye orodha hiyo kwa sababu ya maumivu ya misuli.
Ilikuwa asafiri kuelekea Shelisheli, lakini imekazimu benchi la ufundi kumuondoa kwa sababu bado hajawa sawa asilimia 100, anahitaji muda wa kujifua zaidi ili kupata utimamu wa mwili tayari kwa mapambano uwanjani , daktari wake pia amethibitisha kuwa mchezaji anatakiwa apate muda wa kujiweka sawa kabla hajaanza kucheza mechi kulingana na majeraha aliyokuwa nayo.
Orodha kamili ya wachezaji ambao safiri kuelekea Shelishelini kama Ifuatavyo:
Ramadhani Kabwili, Beno Kakolanya, Youthe Rostand, Hassan Kessy, Juma Abdul, Mwinyi Haji, Gadiel Michael, Nadir Hariub, Patto Ngonyani, Kelvin Yondani, Said Juma, Papy Tshishimbi,Pius Buswita, Raphael Daud, Yussuf Mhilu, Ibrahim Ajib, Said Mussa, Emmanuel Martin, Godffrey Mwashiuya, Juma Mahadhi.

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: Nyota Hawa 20 Wa Yanga SC kuelekea Shelisheli Kesho Tayari Kuivaa St Louis, Chirwa ‘Out’
Nyota Hawa 20 Wa Yanga SC kuelekea Shelisheli Kesho Tayari Kuivaa St Louis, Chirwa ‘Out’
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhavudyXqu4ROKZtCeuNj2h5B_M8tMQmrnzN0xwHyuoVq3EFq1fPXJ-Lw1QQ1fbENU65VqK_HeuVqWK5FRsFXu9N-cvPcjU6sMuYHdTfDb-gqNxFz4qXJmWZFXh0XExGMRDhmjkw_7wgJtM/s640/ten-.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhavudyXqu4ROKZtCeuNj2h5B_M8tMQmrnzN0xwHyuoVq3EFq1fPXJ-Lw1QQ1fbENU65VqK_HeuVqWK5FRsFXu9N-cvPcjU6sMuYHdTfDb-gqNxFz4qXJmWZFXh0XExGMRDhmjkw_7wgJtM/s72-c/ten-.jpg
Habari Today
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/nyota-hawa-20-wa-yanga-sc-kuelekea.html
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/nyota-hawa-20-wa-yanga-sc-kuelekea.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy