Raisi Wa Zamani Wa LIBERIA ELLEN JOHNSON SIRLEAF Ashinda Tuzo Ya Kiongozi Bora Wa Africa Inayotolewa Na MO IBRAHIM

Rais wa zamani wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf ameshinda tuzo ya mwaka ya Mo Ibrahim kwa Uongozi wa Afrika – ambayo hupewa viongozi w...


Rais wa zamani wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf ameshinda tuzo ya mwaka ya Mo Ibrahim kwa Uongozi wa Afrika – ambayo hupewa viongozi wa Afrika ambao wameonekana kuwa na utawala mzuri. 

Ellen Johnson Sirleaf amekuwa mwanamke wa kwanza barani Afrika kushika nafasi ya Urais mwaka 2006 na kumaliza muda wake mwezi uliopita baada ya kuhudumu kwa mihula miwili.
Kamati ya Utendaji ya tuzo ya Mo Ibrahim imesema Ellen Johnson Sirleaf ameonesha uongozi wa kipekee katika kukabiliana na changamoto zisizowahi kutokea katika awamu zake mbili za uongozi alipokuwa Rais wa Liberia.


Wakati aliposhinda uchaguzi wa Rais nchini humo mwaka 2005, nchi hiyo ilikuwa imegawanyika kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa miaka kadhaa na tuzo hiyo ya amani ilikuwa ni kwa ajili ya kumpongeza kusaidia kuiimarisha nchi hiyo.


Wakosoaji wake wamekuwa wakimkosoa kwa kuwa na upendeleo, kutokana na kuwachagua watoto wake katika nafasi za ngazi za juu na pia wanadai kuwa hakuchukua hatua za kutosha kupambana na rushwa.
Kamati yab utendaji ya Mo Ibrahimu imearifu kwamba inafahamu mapungufu yake, lakini imeamua kwamba anastahili kupata tuzo ya dola za kimarekani milioni 5.
Mjasiriamali Mwingereza mwenye asili ya Sudan Mo Ibrahim alianzisha tuzo hiyo mwaka 2007 kwa ajili ya kuwatunukia viongozi walionesha kazi nzuri wakati wa kipindi cha uongozi wao ndani ya bara la Afrika, amballo madikteta na watawala wadhalimu wamerudisha nyuma maendeleo ya bara hili.
Tuzo hii ambayo inapaswa kutolewa kila mwaka , kwa mara sita mfululizo ilishindwa kupata mtu, kutokana na viongozi kukosa sifa za kushinda tuzo hiyo.

Ellen Johnson Sirleaf atapata dola za Kimarekani milioni tano zitakazogawanywa kwa miaka kumi, na dola laki mbili kwa maisha yake yote.

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: Raisi Wa Zamani Wa LIBERIA ELLEN JOHNSON SIRLEAF Ashinda Tuzo Ya Kiongozi Bora Wa Africa Inayotolewa Na MO IBRAHIM
Raisi Wa Zamani Wa LIBERIA ELLEN JOHNSON SIRLEAF Ashinda Tuzo Ya Kiongozi Bora Wa Africa Inayotolewa Na MO IBRAHIM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjgMW_tmtZf6_zvF_bQUx1e3phIUExKrKimFvKC8alFt1hcQ729pTQavb24vEOYcTu-CguTv054lJXDWOzZy1RV9mpk5uMwtoc-vtnEsV1fWb27ByILZ2cUh-l6LEN-FutJffa_-WuDsa4c/s640/Ellen-Jonhson.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjgMW_tmtZf6_zvF_bQUx1e3phIUExKrKimFvKC8alFt1hcQ729pTQavb24vEOYcTu-CguTv054lJXDWOzZy1RV9mpk5uMwtoc-vtnEsV1fWb27ByILZ2cUh-l6LEN-FutJffa_-WuDsa4c/s72-c/Ellen-Jonhson.jpg
Habari Today
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/raisi-wa-zamani-wa-liberia-ellen.html
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/raisi-wa-zamani-wa-liberia-ellen.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy