RC Makonda Apiga Marufuku Ukamataji Hatarishi Wa Bodaboda Dar

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda ametoa onyo kali kwa kampuni zinazofanya kazi ya kukamata Pikipiki (bodaboda) kwa mtindo ...


Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda ametoa onyo kali kwa kampuni zinazofanya kazi ya kukamata Pikipiki (bodaboda) kwa mtindo wa kuvamia kitendo kinachohatarisha usalama wa Dereva na Abiria.
A post shared by Paul Makonda (@paulmakonda) on

RC Makonda amesema zipo baadhi ya kampuni zimekuwa zikivizia madereva wa Bodaboda kisha kuwavamia na kuwakamata na wakati huohuo kuwapiga kitendo ambacho amesema hawezi kukiruhusu kiendelee kwenye Mkoa wake.

Mhe. Makonda ametoa onyo hilo wakati wa kikao na Madalali wanaotekeleza hukumu za Mahakama na Bank kilicholenga kuwatambua na kupitia nyaraka zinazowapa mamlaka ya kufanya kazi hiyo ili Wasionekane Matapeli na waweze kupata ushirikiano wa serikali.


Uamuzi wa RC Makonda kukutana na madalali hao ni manyanyaso na ukandamizaji unaofanywa na baadhi ya madalali wanaopiga minada Nyumba, Magari, Viwanja, Mashamba, Ofisi na Mali za watu bila kufuata taratibu na kusababisha maumivu makali kwa wananchi.

Amesema zipo kampuni za udalali zinazofoji nakala za hukumu, mihuri, sahihi za mahakama,ofisi ya Mkoa, Wilaya na Mitaa na wakati mwingine kufanya minada bila kufuata taratibu.


Baadhi ya wamiliki wa kampuni za udalali

Kutokana na hilo RC Makonda amezitaka kampuni zote za udalali Dar es salaam kuwasilisha nakala za nyaraka ya usajili kwa mwanasheria wa mkoa zipitiwe na kujiridhisha ili wapewe ushirikiano na Serikali.


Nao Madalali wamemshukuru RC Makonda kwa uamuzi wa kuwatambua ili wapate ushirikiano wa Serikali kwakuwa wapo baadhi ya madalali waliokuwa wakifanya kazi hiyo kinyume na sheria na kuwachafulia kazi wale wenaofata taratibu za kazi hiyo.

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: RC Makonda Apiga Marufuku Ukamataji Hatarishi Wa Bodaboda Dar
RC Makonda Apiga Marufuku Ukamataji Hatarishi Wa Bodaboda Dar
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjRinYwIQojF9eiSKUYJTxgm2AYDUP5zlhdYeWYY6lFch7DoOSvfhDefIzIGXFBia0ZPOq4bYo9d45qviUSuZ-1eFJPehflGcL5M4RF-DTc1RLYoFT52R_JiT3eS6Nvxx1YlzDAsGwSwnGC/s640/kondaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjRinYwIQojF9eiSKUYJTxgm2AYDUP5zlhdYeWYY6lFch7DoOSvfhDefIzIGXFBia0ZPOq4bYo9d45qviUSuZ-1eFJPehflGcL5M4RF-DTc1RLYoFT52R_JiT3eS6Nvxx1YlzDAsGwSwnGC/s72-c/kondaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.jpg
Habari Today
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/rc-makonda-apiga-marufuku-ukamataji.html
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/rc-makonda-apiga-marufuku-ukamataji.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy