Sakata La YANGA Uwanja Wa Taifa Latua Bungeni

Sakata la Klabu ya Yanga kuzuiliwa kufanya mazoezi katika uwanja wa Taifa lililotokea siku ya jana (Alhamisi) limezua sura mpya na kufa...


Sakata la Klabu ya Yanga kuzuiliwa kufanya mazoezi katika uwanja wa Taifa lililotokea siku ya jana (Alhamisi) limezua sura mpya na kufanya Waziri mwenye dhamana Dkt. Harrison Mwakyembe kulitolea ufafanuzi Bungeni.
Dkt. Mwakyembe ametoa ufafanuzi huo leo (Ijumaa) katika mkutano wa 10 kikao cha nane cha Bunge kilichomalizika kwa kuhairishwa shughuli zake mpaka Aprili 03, mwaka 2018 mjini Dodoma wakati alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mchinga (CUF), Hamidu Bobali ambapo aliitaka serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo iingilie kati suala la timu za Tanzania zikienda kucheza kimataifa huwa zinawekewa zengwe lakini wao wakija kucheza huku wanapewa kipaumbele baadhi ya vitu.
"Haturuhisiwi hicho kiwanja kukitumikisha kubeba michezo zaidi ya mitatu kwa wiki moja na endapo utafanya hivyo unaingiza uswahili na hata kikiharibika huwezi kwenda kudai kwa mtu aliyekupa 'guranty' kwamba kitaka zaidi ya miaka 10", amesema Dkt. Mwakyembe.
Pamoja na hayo, Dkt. Mwakyembe ameendelea kwa kusema "kwa hiyo wiki hii tuna mechi mbili muhimu kesho (Jumamosi) wanacheza Yanga dhidi ya St. Louis na kesho kutwa wanaingia Simba SC (Jumapili) kucheza na timu kutoka Djibout. Kanuni za kimataifa zinataka timu ngeni hiyo ya kimataifa lazima ifanye mazoezi katika kiwanja ambacho kitachezwa mechi hiyo lakini hata FIFA wanatambua hicho kiwanja ni cha timu za hapa nchini. Kwa hiyo Yanga na Simba wanaufahamu vizuri uwanja huo ndio maana wakapewa kipaumbele wageni ili waweze nao kuujua".
Aidha, Dkt. Mwakyembe amesema anahisi kuna uswahili umeshaanza kuingia katika uwanja wa Taifa na kutaka baadhi ya watu kushughulikiwa.
"Uswahili umeshaanza kuingia katika uwanja wetu wa Taifa, na mimi nashukuru kwa haya maneno niliyoyapata nadhani kuna vijana wangu pale wanahitaji wadhibitiwe kwa kweli. Kwa hiyo nataka nifafanue kwamba ni haki ya wageni wapewe nafasi ya kufanya mazoezi na sisi tukafanyie katika viwanja vingine", amesisitiza Dkt. Mwakeymbe.

 Kwa upande mwingine, Dkt. Mwakyembe amesema ili uwanja huo uweze kutunzika katika mazingira mazuri bila ya kuharibiwa jambo lolote ndani ya miaka 10 ni lazima yawepo masharti ya utumiaji.

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: Sakata La YANGA Uwanja Wa Taifa Latua Bungeni
Sakata La YANGA Uwanja Wa Taifa Latua Bungeni
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhIVrMcU6okIKLAkhD5U4iNehMWKCw-NXFvx6M5fzmsqZcKs48a_lxQf03bkobjsSHhudr6yCpZ-fj_acoU8O6UfB8RNVM4a28yIuPg5G2-8OHPD4WwadBhyzBaqDGjv_amIzSYjdQbXVMj/s640/yangaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.PNG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhIVrMcU6okIKLAkhD5U4iNehMWKCw-NXFvx6M5fzmsqZcKs48a_lxQf03bkobjsSHhudr6yCpZ-fj_acoU8O6UfB8RNVM4a28yIuPg5G2-8OHPD4WwadBhyzBaqDGjv_amIzSYjdQbXVMj/s72-c/yangaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.PNG
Habari Today
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/sakata-la-yanga-uwanja-wa-taifa-latua.html
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/sakata-la-yanga-uwanja-wa-taifa-latua.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy