Serikali imesema ina andaa mikakati itakayowezesha kudhibiti biashara ya ngono na uwepo madanguro nchini, hasa kwenye maeneo ya mijini...
Serikali imesema ina andaa mikakati
itakayowezesha kudhibiti biashara ya ngono na uwepo madanguro nchini,
hasa kwenye maeneo ya mijini.
Hayo yamesemwa jana Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile
wakati akijibu swali la Mbunge wa Mtambwe, Khalifa Mohammed Issa
aliyehoji juu mpango serikali katika kudhibiti biashara ya ngono na
madanguro ili kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (VVU)
nchini.
Akijibu swali la Issa, Dkt. Ndugulile alisema Serikali inaandaa mikakati
mbalimbali ikiwemo utoaji wa elimu kuhusu madhara ya biashara ya ngono
kwa jamii pamoja na kuchukua hatua za kisheria kwa wanaojihusisha na
baishara hiyo, pamoja na kudhibiti uwepo wa madanguro.
Katika hatua nyingine, Dkt. Ndugulile alisema serikali inaendelea
kuchukua hatua katika kudhibiti mila na desturi potofu zinazochangia
maambukizi mapya ya VVU, ikiwemo ukeketaji na urithishaji wa wajane kwa
ndugu wa mume, kwa kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara ya mila potofu
pamoja na kutoa hamasa kwa wakunga wa jadi wanaojihusisha na ukeketaji.
COMMENTS