Wakati Serikali ya Tanzania na nchi nyingine barani Afrika zikihimiza ulazima wa tohara kwa wanaume, hii ni tofauti kabisa na nchi ya ...
Wakati Serikali ya Tanzania na nchi
nyingine barani Afrika zikihimiza ulazima wa tohara kwa wanaume, hii ni
tofauti kabisa na nchi ya Iceland ambapo limetangaza kupiga marufuku
tohara kwa wanaume na kuwa taifa la kwanza barani Ulaya kufanya hivyo.
Hata hivyo mvutano wa kupitisha
muswada huo bado unajadiliwa bungeni huku kukiwa na mvutano wa kidini
kati ya Wayahudi na Waislamu ambao ndio wachache kwenye bunge hilo.
Kwa mujibu wa gazeti la
Times Of Israel
limeeleza kuwa Muswada huo unaojadiliwa na Bunge la Iceland
unapendekeza kwa mtu yeyote atakayekutwa amefanyiwa tohara afungwe hadi
miaka sita jela la sivyo awe na sababu maalumu za kufanyiwa tohara.
Kwa upande mwingine Wanaharakati na Wanadiplomasia duniani wamesema
kuwa hatua hiyo itazua hisia kali kwa viongozi wa kidini barani Ulaya
huku wakieleza kuwa Wayahudi na Waislamu ambao ni zaidi ya 2,000+ nchini
Iceland watakuwa katika hali ngumu ya maisha.
Wabunge wengi wanaounga mkono muswada huo Muswada huo wanasema kuwa
tohara ya wavulana wadogo inakiuka haki yao ya kibinaadamu na ni kinyume
na azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki ya mtoto.
Ingawaje kwenye muswada huo kuna kipengele kinachoruhusu mwanaume
kufanyiwa tohara kwa sababu za kidini au afya kwa masharti ya hadi
afikie miaka 18, Waislamu na Wayahudi wanapinga vikali hatua hiyo kwani
inakiuka tamaduni yao ya kuwafanyia tohara watoto wadogo.
Chanzo:The Guardian & Times Of Israel
COMMENTS