Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imebaini mambo matano baada ya kumchunguza Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Followship (FG...
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imebaini mambo matano baada ya
kumchunguza Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Followship
(FGBF), Zachary Kakobe, ikiwemo kukwepa kodi na kuhifadhi mabilioni ya
fedha katika majaba na ndoo.
Mambo yaliyobainika baada ya kufanyika kwa uchunguzi huo
Imesema Askofu huyo hana akaunti wala fedha katika taasisi ya fedha hapa nchini. Aidha uchunguzi ulibaini kuwa Askofu Kakobe ni mmoja wa wasimamizi wakuu wa akaunti za kanisa zilizopo katika benki ya NBC zenye jumla ya kiasi cha Sh8.2bilioni, kiasi hiki cha fedha kimetokana na sadaka, zaka na changizo ambazo zinatolewa na waumini wa kanisa tajwa hapo juu, hivyo kwa mujibu wa sheria hakitozwi kodi.
Kampuni inayomilikiwa na watoto wa Askofu Kakobe ilikwepa kulipa kodi ya Sh37.2 ambazo zimelipwa baada ya uchunguzi. Kwa ujumla kiasi kilicholipwa kutokana na uchunguzi ni Sh58.1milioni.
Kanisa linatunza kiasi kikubwa cha fedha kwenda ndoo na ‘majaba’ kinyume na taratibu za utunzaji fedha.
COMMENTS