Viwanja Vya Ndege 11 Nchini Tanzania Kufanyiwa Ukarabati

Serikali imeanza majadiliano na Benki ya Dunia ili kupata mkopo wa kugharamia ukarabati na upanuzi wa Viwanja vya Ndege 11 kwa kuzingati...


Serikali imeanza majadiliano na Benki ya Dunia ili kupata mkopo wa kugharamia ukarabati na upanuzi wa Viwanja vya Ndege 11 kwa kuzingatia mapendekezo ya ripoti ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ambao ulizingatia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ukuaji wa shughuli za kiuchumi, utalii na mahitaji ya usafiri wa anga.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Ndikiye Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Tanga Mhe. Mussa Mbarouk lililohusu Ujenzi wa Uwanja wa Ndege mkubwa na wa kisasa katika jiji la Tanga.
Mhandisi Ndikiye amesema kuwa kiwanja cha ndege cha Tanga ni miongoni mwa viwanja hivyo 11 vilivyofanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa kugharamiwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa Transport Sector Support Project (TSSP).

“Katika upembuzi huo kiwanja cha ndege cha Tanga ni miongoni mwa viwanja vilivyopewa kipaumbele kwa mahitaji ya ukaribu hivyo katika majadiliano ya awali Benki ya Dunia imeonesha nia ya kugharamia ukarabati wake.”

“Kwa sasa majadiliano kati ya Serikali na Benki ya Dunia yanaendelea yakiwemo mapitio ya awali ya ripoti za miradi iliyopendekezwa pamoja na maandalizi ya taarifa mbalimbali zinazohitajika kabla ya mkataba wa mkopo kusainiwa na baadaye kutangaza zabuni,” amefafanua Mhandisi Ndikiye.


Hata hivyo, Mhandisi Ndikiye alivitaja viwanja vingine vilivyofanyiwa upembuzi yakinifu ikiwemo Lake Manyara, Musoma, Iringa, Songea, Kilwa Masoko, Lindi, Moshi, Njombe, Simiyu na Singida ambapo usanifu huo ulimalizika mwezi June 2017 kwa kuhusisha usanifu wa miundombinu ya viwanja hivyo kwa ajili ya upanuzi na ukarabati ili kukidhi mahitaji ya sasa.

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: Viwanja Vya Ndege 11 Nchini Tanzania Kufanyiwa Ukarabati
Viwanja Vya Ndege 11 Nchini Tanzania Kufanyiwa Ukarabati
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifZHbcnraMCxs8e-HNrO1uAFigbnkX_R6_o7Fee5d3D4unqEyFk-3G2nN_PB74R2bGIsFTh6w-ivX0t96ZoO_1jdv-Otzv4zBAS7PQyfXk3-ymTaKsC15ZhvuqTfLQLQw1n9EfC_KdAgHY/s640/1-74.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifZHbcnraMCxs8e-HNrO1uAFigbnkX_R6_o7Fee5d3D4unqEyFk-3G2nN_PB74R2bGIsFTh6w-ivX0t96ZoO_1jdv-Otzv4zBAS7PQyfXk3-ymTaKsC15ZhvuqTfLQLQw1n9EfC_KdAgHY/s72-c/1-74.jpg
Habari Today
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/viwanja-vya-ndege-11-nchini-tanzania.html
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/viwanja-vya-ndege-11-nchini-tanzania.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy