Wavuruga Elimu KONDOA Wamkera Mkuu Wa Wilaya

Mkuu wa Shule ya Sekondari Kwapakacha Mwalimu Pantaleo akisoma barua katika kikao cha wadau wa elimu iliyoandikwa na mwanafunzi wa kid...


Mkuu wa Shule ya Sekondari Kwapakacha Mwalimu Pantaleo akisoma barua katika kikao cha wadau wa elimu iliyoandikwa na mwanafunzi wa kidato cha pili akielezea sababu za kutaka kuacha shule.


 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kondoa akimwelekeza Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Tungufu kupandisha ufaulu baada ya kupokea cheti cha shule yenye ufaulu duni Wilayani katika kikao cha wadau wa elimu kilichofanyika katika ukumbi wa Kondoa Irangi hivi karibuni.


Katibu Tawala Wilaya ya Kondoa, Winnie Kijazi akimpa zawadi mmoja ya walimu waliofaulisha kwa alama A katika mtihani wa darasa la saba mwaka 2017 kwenye kikao cha wadau wa elimu.

Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mh. Sezaria Makota amesema hatowafumbia macho wale wote wenye nia ya kuishusha wilaya ya Kondoa kielimu kwa kuvuruga kwa makusudi mikakati ya kuinua elimu wilayani humu.

Aliyasema hayo wakati wa kikao cha wadau wa elimu wa Halmashauri ya Mji Kondoa kilichofanyika katika ukumbi wa Kondoa Irangi hivi karibuni na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa elimu ili kujadili changamoto na  mikakati ya kuinua elimu ndani ya Wilaya ya Kondoa.
Alisema kuwa katika utawala wake hatoruhusu elimu kushuka kwani matokeo ya darasa la saba mwaka jana wilaya imeshuka kiwastani ukilinganisha na mwaka juzi ambapo wilaya ilikuwa na wastani wa asilimia 80 na mwaka jana imeshuka na kufikia asilimia 71 hivyo viongozi wajipange kusimamia elimu ili kuhakikisha ufaulu unapanda.

Aidha aliwaagiza maafisa elimu kumpelekea mipango yao ili kuona jinsi gani wanainua elimu na kutaka viongozi wa Halmashauri kuacha migogoro na kutekeleza mipango kwa vitendo ili kufikia mafanikio katika elimu.

Wakiongea wadau mbalimbali waliojitokeza walisema kuwa changamoto kubwa ya kushusha ufaulu katika wilaya ni upungufu wa walimu, wazazi kutokuwa na mwamko wa elimu, kukosekana kwa mafunzo kwa walimu, kutolipa madai ya walimu mapema na utoro wa wanafunzi kutokana na kutoelewa masomo.

Hata hivyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kondoa Mh. Hamza Mafita alifafanua kuwa Halmashauri inaendelea kujipanga kuboresha sekta ya walimu kwa kuwapatia motisha walimu na kuwapatia gari Idara ya Elimu ili waweze kufanya ufuatiliaji wa elimu na kuwaagiza Waheshimiwa Madiwani kuweka elimu kuwa agenda ya kudumu katika vikao vya kata.
Akifunga kikao hicho Mbunge wa Kondoa Mjini Mh. Edwin Sannda alisema kuwa viongozi wanawajibu wa kuwabadilisha wazazi ili wawe na utamaduni wa kupenda elimu ikiwa ni pamoja na kuzingatia maadili kwa wanafunzi, walimu na watumishi kwani kwa kufanya hivyo elimu itapanda kwani changamoto zilizopo ni za nchi nzima.

Kikao cha wadau wa Elimu kilifanyika hivi karibuni wilayani Kondoa kwa ajili ya kubaini, kujadili changamoto na kuweka mikakati ya kuinua elimu ambapo pia walimu mbalimbali wa Shule za Masingi waliofaulisha kwa alama A kwa somo walipewa zawadi ikiwemo shule tano zilizofanya vizuri na shule tano zilizofanya vibaya.

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: Wavuruga Elimu KONDOA Wamkera Mkuu Wa Wilaya
Wavuruga Elimu KONDOA Wamkera Mkuu Wa Wilaya
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6ma2nTpv46PRR7sPUF2mhu0vt9b7wKjbb9nyXOKQaS5P2Wk9Uz7V72WFasOxjphIsWpT0AurPQbgwUASt2fWzHHnwxrpQaLLiyJ4JoyiRSRCoSp9WEMsZXL8bs7RXxFYbkmgky1VMmJ3p/s640/el+1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6ma2nTpv46PRR7sPUF2mhu0vt9b7wKjbb9nyXOKQaS5P2Wk9Uz7V72WFasOxjphIsWpT0AurPQbgwUASt2fWzHHnwxrpQaLLiyJ4JoyiRSRCoSp9WEMsZXL8bs7RXxFYbkmgky1VMmJ3p/s72-c/el+1.JPG
Habari Today
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/wavuruga-elimu-kondoa-wamkera-mkuu-wa.html
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/wavuruga-elimu-kondoa-wamkera-mkuu-wa.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy