Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu huenda akashtakiwa na Polisi nchini humo kwa mashtaka ya rushwa. Polisi wamesema kuwa wana u...
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin
Netanyahu huenda akashtakiwa na Polisi nchini humo kwa mashtaka ya
rushwa. Polisi wamesema kuwa wana ushahidi wa kutosha kumtia hatiani
kiongozi huyo kwa rushwa, ufisadi na kuvunjwa uaminifu.
Netanyahu anatuhumiwa kutaka gazeti la Yediot Aharonot kuchapisha
taarifa yake yenye upendeleo ili kuliwezesha gazeti hilo kuweza
kushindana na magazeti mengine kibiashara. Madai mengine ni kwamba
kiongozi huyo alipokea zawadi ya dola 283,000 kutoka kwa msanii wa
Hollwood Mogul Arnon Milchan ili kuweza kumsaidia kupata Visa ya
Marekani.
Polisi wanasema mhariri wa gazeti la Yediot Aharonot, Arnon Mozes na
Milchan ambaye ni mtayarishaji wa filamu nao pia watashtakiwa kwa tuhuma
za rushwa.
Hata hivyo Benjamin Netanyahu amekanusha tuhuma hizo na kusema madai
hayo hayana msingi wowote na ataendelea kuwa Waziri mkuu wa nchi hiyo,
wakati huo huo vyombo vya habari nchini humo vikieleza kuwa tayari
Netanyahu amehojiwa mara zisizopungua saba.
COMMENTS