YANGA Kuanza Mbio Za Klabu Bingwa AFRIKA Leo TAIFA

YANGA FC Saint Louis Suns United Yanga SC leo wanatupa kete yao ya kwanza katika michuano ya Ligi Mabingwa Afrika watakapomenyana ...


YANGA FC

Saint Louis Suns United

Yanga SC leo wanatupa kete yao ya kwanza katika michuano ya Ligi Mabingwa Afrika watakapomenyana na Saint Louis Suns United ya Shelisheli katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mchezo huo unatarajia kuwa mwepesi kwa upande wa Yanga kutokana na timu ya St Louis haina uzoefu wowote katika michezo ya kimataifa hasa hii michezo ya vilabu Bingwa Afrika.
Yanga leo inaanza mchezo wao wa kwanza kuwania kombe hilo la Klabau Bingwa Afrika kwenye raundi ya kwanza ya mtoano ikimkosa mshambualiaji wake hatari, Amissi Tambwe.

Amissi Tambwe, licha ya kupata nafuu ya majeraha yake ya goti, ameondolewa katika kikosi cha timu yake na kutakiwa kufanya mazoezi mepesi ya binafsi.

Tambwe, raia wa Burundi, ameongezewa wiki moja ya kuhakikisha hali yake inaimarika zaidi.
Daktari wa Yanga, Edward Bavu amesema Tambwe ameongezewa siku hizo baada ya kulalamikia maumivu wakati akifanya mazoezi magumu juzi.

Bavu alisema baada ya kumfanyia vipimo na kuonekana bado hayupo fiti, amemuongezea muda wa kukaa nje ya uwanja na kufanya mazoezi mepesi ya binafsi.
“Tunataka Tambwe akirejea uwanjani awe fiti kwa asilimia kubwa na hiyo ni baada ya hivi karibuni kulalamikia kusikia maumivu wakati anafanya mazoezi na wenzake.

“Ninaamini baada ya wiki moja atarejea uwanjani kwani hivi sasa anapata matibabu huku akiendelea na mazoezi binafsi kwa ajili ya kuwa fiti na kurejea uwanjani haraka,” alisema Bavu.
Wakati huohuo, Bavu alisema beki wa kati wa Yanga, Andrew Vincent ‘Dante’, ameanza kupata nafuu ya kufanya mazoezi ya ufukweni baada ya kusumbuliwa na maumivu ya misuli.

Wawakilishi wengine wa Tanzania kwenye michuano hiyo, Zimamoto ya Zanzibar ambayo leo inaikaribisha Wolaitta Dicha wa Ethiopia Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

COMMENTS

Name

Entertainment,110,Fashion,5,Health,5,Job,11,Lifestyle,2,Makala,6,Music,4,News,177,Sports,98,Videos,14,
ltr
item
Habari Today: YANGA Kuanza Mbio Za Klabu Bingwa AFRIKA Leo TAIFA
YANGA Kuanza Mbio Za Klabu Bingwa AFRIKA Leo TAIFA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjvXrOQUFIrzIzuhTuY1HYc9_WrF3mBGdO7nTHXM5-LUH0-LD88qMsLNVcfY44NshyphenhyphenuPbnKXkl3o-3ePQFnYnkQfCGqKuF0bm0WN3uIi_XHJKp3DNAhHz3zxry0XMI84wBOh1HsdeOimndz/s640/New-Yanga.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjvXrOQUFIrzIzuhTuY1HYc9_WrF3mBGdO7nTHXM5-LUH0-LD88qMsLNVcfY44NshyphenhyphenuPbnKXkl3o-3ePQFnYnkQfCGqKuF0bm0WN3uIi_XHJKp3DNAhHz3zxry0XMI84wBOh1HsdeOimndz/s72-c/New-Yanga.jpg
Habari Today
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/yanga-kuanza-mbio-za-klabu-bingwa.html
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/
http://habaritodaytzz.blogspot.com/2018/02/yanga-kuanza-mbio-za-klabu-bingwa.html
true
7010127043980995099
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy